JOGOO WA SHAMBA : EPISODE 01

                               JOGOO WA SHAMBA: Episode 01
   Shauri ni kijana wa kwanza kuzaliwa katika familia ya watoto watatu,kazaliwa kutoka katika familia ya kimaskini  yeye na  wadogo zake Fadhil na Justine, na ni wakazi wa mkoa wa Mbeya. Baba yao alifariki na mama yake alikuwa ni mkulima mdogo asiye na uwezo wa kumudu baadhi ya mahitaji ya familia.Kijana Shauri alikuwa na bidii sana katika kazi mbali mbali za nyumbani na shule japo majukumu ya nyumbani yalimzidia na wakati mwingine alilazimika kwenda shamba kumsaidia mama yake shuguli za shamba badala ya kwenda shule.Walimu wake hawakujua tatizo lake hivyo alikabiliwa na adhabu kila alipokosekana shule.Kijana Shauri alijitahidi sana kuwasaidia wadogo zake katika shughuli za nyumbani kama vile kufua,kuwaogesha na kuwapikia.
    Baada ya miaka kadhaa kijana alihitimu shule ya msingi na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule ya kata pale kijijini kwao, kijana alichelewa kuanza kidato cha kwanza kutokana na changamoto ya kiuchumi lakini hata hivyo alijiunga na wenzake na kuanza masomo rasmi mwezi wa pili, kijana alisoma kwa bidii na pamoja na misukosuko mingi alijikuta akipendwa sana na walimu sababu ya kujituma kwake ndani na nje ya darasa.alipofika kidato cha tatu mdogo wake wa pili aitwaye fadhil nae alijiunga na kidato cha kwanza hivyo kufanya mambo kuwa magumu sana kwa mamayao kwani hakuweza kumudu gharama za kuwasomesha watoto wawili hivyo ikamlazimu kijana Shauri kuanza kufanya vibarua mbalimbali mtaani kwaajili ya kutafta pesa za karo yake na ya madogo wake hata hivyo kijana alifanikiwa kuingia kidato cha nne. Akiwa kidato cha nne kijana alisoma kwa bidii sana na hatimaye alihitimu.
    Baada ya muda matokeo yalitoka na yakawa mazuri kijana alifaulu kujiunga na kidato cha tano katika shule moja mkoani Kigoma,kijana alihangaika huku na kule kutafuta msaada hatimaye alipata ufadhili wa mtu binafsi aliyejitolea kumsomesha.Kijana alijiunga na kidato cha tano na baada ya muhula mmoja kwa bahati mbaya alipata taarifa za kifo cha mfadhili wake.Shauri alilia sana huku akijiuliza ni kwa namna gani ataweza kusoma tena kwani mama yake hakuwa na uwezo kabisa,na tangu Shauri aende shule hakuwahi kurudi nyumbani kutokana na changamoto ya nauli.kijana alimshirikisha Mwalimu wake juu ya tatizo hill na mungu si athumani Mwalimu aka ahidi kumsaidia kulipa karo.Pamoja na misukosuko yote kijana alisoma kwa bidii sana na kufaulu vema kwenye masomo yake na hatimaye alihitimu kidato cha sita.Kijana alimshukuru sana Mwalimu wake kisha akasaidiwa nauli na kurudi nyumbani ambako familia yake walimpokea kwa Furaha sana ndugu yao.Kwa kuwa ulikuwa msimu wa kilimo kijana alimsaidia sana mama yake katika shughuli za shamba kwa kipindi chote cha kusubili majibu, na hatimaye majibu yalitoka yakiwa mazuri kijana kafaulu kuingia chuo kikuu.Alifurahi sana ila ghafla akaingiwa na huzuni baada ya kukumbuka adha za karo alipokuwa shule.Kwa bahati nzuri kijana alipata mkopo hivyo akajiunga na chuo kikuu cha Dar es salaam akisomea shahada ya sheria.Akiwa anakaa hostel alipata kufahamiana na marafiki kadhaa na kubwa zaidi alianza kuona watoto wakike wazuri ambao kijijini kwao hakufanikiwa kuwaona,Hakika alitaman naye sikumoja awe na mpenzi kama wenzie walivofanya.Katika kikundi cha kujisomea Kwa bahati nzuri nae  alifahamiana na mdada mmoja aitwaye victoria mtoto aliyetoka katika familia ya kitajiri.walipata kuwa marafiki kwa muda kisha binti alinza kuingiwa na hisia za mapenzi kwa kijana Shauri ambaye hakuwa na mvuto kwa wadada wengi kwani hakuwa mtanashati kama wana chuo wengine,kijana alivalia mavazi makuukuu kutokana na kutokuwa na uwezo wa kununua mavazi mapya.
Victoria alishindwa kuzuia hisia zake kwa bwana Shauri huruma ilimuingia baada ya kusimulia siku moja historia ya maisha yake akajikuta akimsaidia Shauri pesa za matumizi pamoja na kumnunulia mavazi mapya hivyo kubadili muonekano wa kijana lakini bado hawakuwa wapenzi kwani hakuna aliye weza kumwambia mwenzake.Baada ya kuingia mwaka wa pili kijana alikosa mkopo kutokana na mabadiliko ya kielimu na hivyo maisha kumuwia magumu,kijana hakusita kumwambia rafiki yake Victoria nae akamtoa wasiwasi na kumsaidia pesa nyingi ambazo alilipa ada na akabakiwa na pesa za kutosha zilizo muweka mjini.
   Baada ya muhula mwingine wa masomo Victoria alimwambia mama yake kuwa kampata rafiki ambaye anategemea aje kuwa mume wake baadaye lakini hakuwahi kumwambia Shauri kuhusu hisia zake.Kijana SHAURI alijua ni urafiki tu na aliogopa kumwambia vick kuwa anampenda kwani aliogopa anaweza kupoteza msaada ikiwa vick hatakuwa tayali kwa uhusiano huo.Alijikuta akianza kumpenda binti nwingie aitwaye Janeth na kwakuwa muonekano wake wa sasa ulikuwa na mvuto kwa wadada wengi,haikumsumbua kumwambia janeth naye alikubali kuwa wawe wapenzi.
   Mtoto wa kitajiri Victoria aliendeleza urafiki na kijana Shauri na kuendeleza msaada wake kwa kijana,huku kijana Shauri akianza kutumia murua kabisa pesa anazopewa na Victoria kutanua au kula na mtoto Janeth.Shauri alifanya siri uhusiano wake huo lakini kwa mtoto Janeth ilikuwa tofauti alijiachia sana na kuwatambulisha marafiki zake,ikumbukwe wakati huu kijana SHAURI alikwishakuwa mjanja akimiliki simu janja na kompyuta kwa msaada wa Victoria, hivyo walikuwa wakipiga picha akiwa na mtoto Janeth na kuziacha kwenye simu janja yake.
    Mtoto Victoria naye hisia zilimzidia akahisi sasa ni wakati mubashara kabisa wa kumwambia kijana Shauri kuwa wawe wapenzi rasmi,binti alijiandaa kisha akamwomba Shauri wakutane hoteli moja hapa jijini siku ya jumamosi ambayo  sio ya masomo,binti alijiandaa mapema siku hiyo kwa kuvaa nyuzi mpya watoto wa mjini wanaita viwalo vipya,marashi ya harufu nzuri na ya bei mbaya sana,nywele zimeandaliwa vema kabisa pamoja na viatu vyake virefu aliwasili hotelini na kumsubili kijana,huku upande wake kijana Shauri yeye kwa upande wake hakuwahi kuingia hoteli kubwa namna ile naye alijiandaa vema siku hiyo akavalia murua mavazi yake mapya aliyonunuliwa na rafiki yake Victoria na kuelekea hotelini........Je! unajua nini kitatokea baada ya shauri kuwasili? Je! Msichana mrembo Vicky atafunguka hisia zake? Na shauri Je! Atakubali amuache Janeth mpenzi wake? Usipitwe na episode ya pili. 

                                   ITAENDELEA Episode O2………

    Written: by Jelly Mbwilo
    Edited :by Masomo Yetutz blogger.
    Approved :by Samuel Ilomo
   visit: www.masomoyetu.co.tz
  

Comments