JOGOO WA SHAMBA SEHEMU YA PILI

                   

                                                                                         JOGOO SHAMBA EPISODE 2

Ilipo ishia "mrembo Vick alimualika kijana Shauri katika hoteli moja ya kifahari,na akawasili akiwa kapendeza kwa kutupia viwalo vya bei mbaya na kupendeza murua kabisa,huku kijana Shauri nae akitokelezea vilivyo"
  "Inaendelea"
     Mrembo Vick alifika mapema hotelini hapo na kumsubiri mpemzi wake huku akiwa anashushia glass ya wine taratiibu,kijana nae aliwasili hotelini na kuelekea moja kwa moja pale alipokuwa ameketi mpenzi wake.Wakakumbatiana kwa bashasha kabisa huku kila mmoja akiwa amejawa na huba juu ya mwenzie kisha wakaketi,Vick akammiminia glass ya wine bwana Shauri kisha wakaanza mazungumzo yao huku wakitazamana usoni.
     Mrembo Vick alimweleza mzee baba Shauri juu ya malengo aliyo nayo juu yake kwamba anatamani waje kufunga ndoa na kuishi pamoja na Shauri pia alimuunga mkono juu ya suala hilo.Wakati mazungumzo ya wapendanao yakiendelea ghafla alikatiza mrembo Janeth akiwa na mwanaume mwingine,ikumbukwe Janeth pia ni mpenzi wa kando wa mzee baba Shauri,basi macho yakamtoka bwana Shauri kama vile kabanwa na mlango ila kwasababu yupo na bibie Vick ikabidi ajifanye yupo sawa.Mrembo Vick hakuwa mchovu alishuhudia kuduwaa kule kwa mpenzi wake kisha akamuuliza kama kuna tatizo bwana Shauri akakanusha kuwa yupo sawa kabisa basi stori zikaendelea.
      Baada ya muda yule mwanaume aliyekuwa na mrembo Janeth alitoka na kwenda zake kisha akabaki Janeth pekeyake na alikuwa akinywa pombe Kali sana na kulewa sana,kwa bahati mbaya Janeth aliinuka na kuanza kutoka nje lakini alipita karibu na walipokuwa wamekaa Shauri na Vick na ghafla akawaona wakiwa wamekaribiana sana,huku bwana Shauri akijiinamia ili asionekane lakini wapi alionekana na moja kwa moja Janeth aliwafata na kuanza kumuhoji bwana Shauri kuwa huyu ni nani huku akionekana kuwa anazidiwa na pombe. Bwanashauri alijaribu kujikausha lakini mrembo aliendelea kuuliza kwa nguvu na kusema maovu yake mengi mbele ya Vick,Shauri alishindwa kujibu chochote kwa aibu na hatimaye mrembo Vick aliinuka na kukimbia nje huku akiwa analia kwa uchungu sana .......je nini kitaendelea je Shauri atamfanya mini Janeth je Vick atachukua uamuzigani usikose episode ya 3..


Comments