FUGA KISASA UNUFAIKE

            TAJILIKA NA UFUGAJI WA KUKU KWA NJIA BORA
              
                                                  UTANGULIZI

Ufugaji wa kuku umekuwa ukifanywa na watu wengi katika jamii,kwa kulenga Zaidi katika kuinua uchumi wao,kutumia kwa  kitoweo na matumizi ya mbolea mashambani na bustanini.Watu hawa hufuga kwa njia ambazo si za kisasa kutokana na kutokua na Elimu juu ya uzalishaji au ufugaji wa kuku.                                    
           Namna Ya Ufugaji Wa Kuku Kwa Njia Bora
         1.Maandalizi ya banda
          Banda linalo stahili katika ufugaji bora ni lile lenye sifa  zifuatazo:-
a.  .Linaruhusu mwanga na hewa kupita{ventilation}
b. Ni kavu muda wowote na haliruhusu unyevu kupita au kupenya kama mvua
c.  Lisiwe lina ruhusu wadudu kama nyoka,nge kupita au kupenya.
d. Liwerahisi kufanya usafi kwa wakati.
e.  Lisikaribiane na banda jingine jirani la kuku ili kuzuia maambukizi ya magonjwa.
      2.Matayalisho Kwa Kuwaweka Kuku Wako Katika Banda
     Matayarisho ya kuwaweka kuku katika banda lako inategemeana na aina ya kuku ambao umewaandaa au umeanzia kuwafuga.
    i.VIFARANGA
 Katika maandalizi ya mahali pakuwaweka vifaranga wenye siku moja au Zaidi panahitaji umakini ili kukwepa au kuondokana na vifo vya vifaranga
 Maandalizi ya Brooder kwaajii ya kulea vifaranga.
a.       Pima eneo la chumba ambacho umekiaandaa katika banda lenye sifa zote na  ujue ukubwa wa eneo katika upana na urefu kwa kutumia tepu.
b.      Na ukijua urefu na upana wa chumba chako chukua urefu zidisha kwa upana uliopata mfano {upana10m*urefu 5=50}.
c.       Ukishapata jumla ya ukubwa wa chumba chako jiulize unataka kufuga vifaranga vingapi kwani kitaalamu vifaranga 10 vinafugwa kwenye mita moja kwa mfano hapo juu mimi nimepata jumla 50mita za chumba changu kwa hivo vifaranga visivyo zidi 50 nahitaji kufuga katika eneo langu.

       Vitu Vinavyo Hitajika Katika Maanadalizi Ya Brooder
        i.            Malanda ya mbao
      ii.            .Mifuko ya nailoni au salufeti.
    iii.            .Majarida
    iv.            Singi board.
Maandalizi ya brooder.
        i.            Chukua kiasi cha Maranda mwaga katika eneo lako ulilo pima na kujua idadi ya vifaranga utakavyo weka Mwaga kiasi cha sentimita 3 hadi 4kutoka chini.
      ii.            Chukua mifuko yako ya nailoni tandika pale ulipo mwaga Maranda.
    iii.            Chukua majarida yako ya tandike juu ya mifuko ya nailoni.
      .
KUPATA NAKALA ZAIDI YA KITABU AU PDF WASILIANA NASI SIMU NAMBA : 0762039071 AU 0625511488 PIA WAWEZA ULIZA SWALI LOLOTE KWA KU COMENT HAPA.



           










Comments